TUNAOMBA KATORO SASA IWE HALMASHAURI

Mbunge wa Katoro, Eng. Kija Limbu Ntemi ameitaka Serikali kueleza hatua zinazohitajika ili Majimbo ya Katoro na Busanda yaweze kupatiwa Halmashauri akisema majimbo hayo yamekidhi vigezo vya kuwa na Halmashauri.
 

Akijibu swali hilo lilioulizwa kwa niaba ya Mbunge huyo, Bungeni Jijini Dodoma leo Agosti 26, 2026, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe amesema uanzishaji wa Halmashauri mpya hufuata Sheria za Serikali za Mitaa pamoja na Mwongozo wa Uanzishwaji wa Maeneo ya Utawala wa mwaka 2025.


Serikali imesema kusudio la kuanzisha Halmashauri mpya linapaswa kujadiliwa na kupitishwa na Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), kabla ya kuwasilishwa na Katibu Tawala wa Mkoa kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa.

Hata hivyo, Serikali imesema hadi sasa kusudio la Majimbo ya Katoro na Busanda kupatiwa Halmashauri bado halijawasilishwa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, hivyo Mamlaka zinazohusika zimetakiwa kuendelea na taratibu kwa kufuata Sheria na Miongozo iliyowekwa.

Post a Comment

0 Comments