Safari
ya ndege ya kampuni ya Porter Airlines nchini Canada imelazimika
kusitisha safari baada ya mtoto mdogo kukataa kufunga mkanda wa usalama
kabla ya kuondoka, hali iliyozua mjadala kuhusu taratibu za usalama kwa
watoto wanaosafiri kwa ndege.
Tukio hilo lilitokea Agosti 6, 2026
wakati ndege hiyo ikiwa imejiandaa kuondoka kutoka Victoria kuelekea
Toronto. Kwa mujibu wa kampuni hiyo, ndege ilirejeshwa katika eneo la
kupandia abiria baada ya mtoto kusimama kwenye kiti chake na kukataa
kufunga mkanda.
Kutokana na hali hiyo, ndege hiyo haikuweza
kuendelea na safari, na abiria walilazimika kupangiwa usafiri mwingine
siku iliyofuata.
Porter Airlines imesema mzazi aliyekuwa
akisafiri na mtoto huyo pamoja na wahudumu wa ndege walijaribu kutatua
suala hilo lakini juhudi zao hazikufanikiwa.
“Katika hali hiyo, ndege isingeweza kuondoka kwa sababu haikuwa salama,” kampuni hiyo imeeleza katika taarifa yake.
0 Comments