Mwenyekiti wa
CHADEMA Tundu Lissu amekutwa na kesi ya kujibu katika kesi ya uhaini
inayomkabili inayoendelea katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ya
Dar es Salaam hivyo sasa anataja mashahidi wake 11 wa kumtetea akiwemo
Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Mstaafu Dkt Philip Mpango
na Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa na IGP Wambura.
Baada ya
kusikiliza pande zote mbili mahakama imeona kwamba baada ya kupitia
ushahidi na maneno yaliyoko kwenye hati ya mashtaka na ushahidi.
Mahakama
imeeleza ushahidi uliotolewa una mzungumza mshitakiwa na kwa mujibu wa
sheria mahakama imeona kuna kesi imejengwa na mahakama inaona kwamba
mshitakiwa ana kesi ya kujibu ili aweze kujitetea dhidi ya tuhuma hizo.
0 Comments