DPP YATAKA MASHAHIDI SABA WA LISSU WAONDOLEWE

Upande wa mashtaka unaoongozwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) umeitaka mahakama Kuu kutowaita baadhi ya mashahidi waliotajwa na mshtakiwa Tundu Lissu Mwenyekiti wa CHADEMA katika kesi ya uhaini inayomkabili.

Baada ya mahakama kumkuta Lissu na kesi ya kujibu, Mwenyekiti huyo alitoa orodha ya mashahidi kumi na mmoja ambao ameiomba mahakama iwaite kwa ajili ya kutoa ushahidi katika kesi hiyo.

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka imesema mashahidi namba 1 hadi 7 wasiruhusiwe kuja kutoa ushahidi.

Mashahidi ambao DPP imetaka wasiitwe ni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais, Philip Mpango, pamoja na Kassim Majaliwa aliyekuwa Waziri Mkuu.

Wa nne ni Camillus Wambura, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania. Wa tano ni Jenerali John Mkunda, Mkuu wa Majeshi Tanzania. Shahidi wa sita ni Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa na Ujasusi (TISS). Shahidi wa saba ni Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Kanali wa Polisi Ramadhani Kindai.

Kuhusu mashahidi watatu wa awali, waendesha mashtaka wamesema hao ni viongozi wa serikali inayomtuhumu Lissu kwa kosa la kutishia Katiba ya nchi.

DPP imeiomba mahakama iuone ushahidi wa mashahidi hawa saba kuwa si muhimu kwa sababu ushahidi wao umeshatolewa na mashahidi wa upande wa serikali ambao ni watumishi wa serikali.

Post a Comment

0 Comments