WATU 46 WAFARIKI DUNIA BAADA YA BOTI KUZAMA NIGERIA

 Takriban watu 46 wamefariki dunia katika jimbo la Sokoto, Kaskazini-Magharibi mwa nchi ya Nigeria baada ya boti kuzama.

Maafisa wanasema boti hiyo ilibeba zaidi ya watu 70, wengi wao wakiwa watoto, ambapo bado operesheni ya uokoaji inaendelea.

Msemaji wa Polisi, Ahmad Rufai, amesema kuwa miili 46 imepatikana karibu na Gorau katika eneo la Gorony.

Rufai ameongeza kuwa watu 16 wameokolewa, huku 15 wakiwa bado hawajapatikana na kueleza kuwa eneo hilo ni gumu kufikika, na vyombo vya usalama pamoja na huduma za dharura vinaelekea eneo la tukio.

Shuhuda mmoja aliliambia Shirika la Habari la Reuters kuwa anaamini watoto waliokuwemo ndani ya boti hiyo walikuwa wakisafiri na wamiliki wa mashamba pamoja na vibarua waliokuwa wakielekea kufanya kazi ya kuvuna mpunga.

Post a Comment

0 Comments