Jeshi
la Polisi Mkoa wa Mara linawashikilia Walimu sita wa Shule ya Sekondari
Makongoro, Wilaya ya Bunda kwa tuhuma za kuhusika na kifo cha
Mwanafunzi wa kidato cha sita, Petro Chisumo (23).
.jpeg)
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, tukio hilo
linadaiwa kutokea Agosti 19, 2026 majira ya saa 11 alfajiri, wakati
Chisumo akiwa pamoja na Wanafunzi wenzake wakitekeleza adhabu baada ya
kupata ufaulu wa chini katika mitihani ya kujipima.
Polisi
imesema katika utekelezaji wa adhabu hiyo, Mwanafunzi huyo alichapwa
viboko na Walimu hao na baadaye kuishiwa nguvu, hali iliyosababisha
kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Bunda kwa matibabu.
Hata hivyo, akiwa anaendelea kupatiwa matibabu, Chisumo alifariki dunia na mwili wake kuhifadhiwa hospitalini hapo.
Jeshi la Polisi limesema sababu halisi ya kifo chake bado inachunguzwa na itatolewa baada ya Madaktari kukamilisha uchunguzi.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mara amewataka Wananchi kuwa watulivu wakati Jeshi
hilo likishirikiana na Wataalamu kutoka Taasisi za kiuchunguzi kubaini
chanzo halisi cha kifo cha Mwanafunzi huyo.
0 Comments