Dunia leo
Jumatano, Agosti 12, 2026, inashuhudia tukio la nadra la kupatwa kwa Jua
kwa jumla, linalotokea wakati Mwezi unapita kati ya Dunia na Jua na
kulifunika Jua kwa muda.
GUSA HAPA,REJESHA HESHIMA YAKO CHUMBANI SASA
Kupatwa kwa Jua kwa jumla kunaonekana
katika maeneo mbalimbali yaliyo kwenye njia ya kivuli cha Mwezi,
yakiwemo Iceland, Greenland, kaskazini mwa Hispania na sehemu ya Ureno.
Katika maeneo hayo, Mwezi utafunika kabisa uso wa Jua na kusababisha
giza la muda mfupi.
Maeneo mengine ya Ulaya na Amerika Kaskazini
yataweza kushuhudia kupatwa kwa Jua kwa sehemu, ambapo Mwezi utafunika
sehemu tu ya Jua. Kiwango cha kupatwa kinatofautiana kulingana na eneo
ambalo tukio hilo linatazamwa.
Kwa upande wa Tanzania, ikiwemo
Dar es Salaam, tukio hilo halitaonekana kwa sababu nchi haipo katika
eneo la mwonekano wa kupatwa kwa Jua leo. Kilele cha kupatwa kwa Jua
duniani kinatarajiwa kufikia karibu saa 17:47 UTC, sawa na saa 2:47
usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Wataalamu wanawashauri watu
watakaokuwa katika maeneo yanayoweza kuona kupatwa kwa Jua kutumia
miwani maalum iliyotengenezwa kwa ajili ya kutazama kupatwa kwa Jua.
Kutazama Jua moja kwa moja bila kinga sahihi kunaweza kusababisha
madhara makubwa kwenye macho.
0 Comments