Shahidi wa 16
wa Jamhuri katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA
Tundu Lissu, ACP Amini Mahamba amemaliza kutoa ushahidi wake leo Agosti
12, 2026 mbele ya Jopo la Majaji watatu wakiongozwa Jaji Dunstan
Ndunguru.
GUSA HAPA,REJESHA HESHIMA YAKO CHUMBANI SASA
Shauri hilo lililopo Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es
Salaam leo liliendelea kwa Lissu kumaliza maswali ya dodoso kwa shahidi
kisha upande wa Jamhuri kuhoji maswali ya kusawazisha (Re-examination)
kwa shahidi huyo.
Shauri hilo limeahirishwa mpaka kesho Agosti
13, 2026 saa tatu asubuhi, hatua ambayo imefikiwa baada ya upande wa
Jamhuri kuomba ahirisho la kesi kwa sababu hawakujiandaa na shahidi
mwingine.
Baada ya ombi hilo la upande wa Jamhuri, Lisu ameiomba
mahakama kusimamia utekelezwaji wa amri ya upande wa Jamhuri kuja na
mashaidi wawili kwa kuwa kesi hiyo imechelewa sana na sio kwa sababu
zake binafsi bali sababu za upande wa Jamhuri hali inayosababisha yeye
kuendelea kukaa gerezani bila hatia.
0 Comments