Mkuu wa Mkoa
wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema baadhi ya Watendaji wazembe
wanasababisha Viongozi watukanwe na Wananchi.
Chalamila ameyasema
hayo leo, Agosti 19, 2026 akiwa katika Stendi ya Kimataifa ya Mabasi ya
Magufuli Jijini Dar es salaam wakati akizungumza kuhusu utekelezaji wa
agizo la kuhamishia mabasi katika stendi hiyo.
Amesema baadhi ya
Watumishi wanadaiwa kuchukua fedha na kutumia nafasi zao kuzorotesha
mchakato wa kuhamisha mabasi kwenda Stendi ya Magufuli.
Amesema
Serikali haitavumilia vitendo vinavyokwamisha utekelezaji wa maagizo
yake, akisisitiza kuwa hatua zitachukuliwa dhidi ya watakaokaidi.
0 Comments