Fabiano Mkeza
ambaye ni Baba wa familia ya Asha Lukonge na Hashim Fabiano ameibua
simanzi wakati wa mazishi ya Mke na Mtoto wake, wanaodaiwa kuuawa kwa
kunyongwa na Ndugu wa familia hiyo, Anderson Bosco.
GY\USA HAPA,REJESHA KUJIAMINI CHUMBANI NA VIKSI LOTION
Mazishi hayo
yamefanyika leo Agosti 18, 2026 katika Makaburi ya Azimio, Kilosa Mjini
baada ya tukio hilo kutokea Agosti 15, 2026 katika Kijiji cha Ilakala,
Kata ya Mhenda, Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro.
Inadaiwa kuwa
tukio hilo lilitokea wakati Fabiano akiwa safarini, ambapo Anderson
ambaye awali alifika katika familia hiyo kwa lengo la kufanya vibarua,
anadaiwa kumuua Asha pamoja na Mtoto wake kwa kuwanyonga, kisha
kuwafukia nyuma ya nyumba yao.
Baada ya tukio hilo, Mtuhumiwa
huyo anadaiwa pia kuuza magunia nane ya mahindi yaliyokuwa yamehifadhiwa
kwa ajili ya chakula kwa shilingi 300,000, ambapo Jeshi la Polisi
limesema linaendelea na msako wa kumtafuta Bosco ambaye anadaiwa
kukimbia baada ya tukio hilo na hadi sasa hajulikani alipo.
0 Comments