Kiungo wa
Hispania Rodrigo Hernández maarufu kama "Rodri" amepokelewa kwa ujumbe
wa kumkaribisha FC Barcelona, huku maneno ya “Benvingut al Barça,
Rodri!” yakitumika kumaanisha “Karibu Barça, Rodri” baada yamefanyika
kusaini mkataba hadi Juni 30, 2030.
Mapokezi hayo yamefanyika leo
huku yakiibua shangwe miongoni mwa Mashabiki wa Barcelona katika
mitandao ya kijamii, huku jina la kiungo huyo likiendelea kuhusishwa na
miamba hiyo ya Hispania.
Rodri amekuwa miongoni mwa viungo
wanaotajwa sana katika soka la Ulaya kutokana na uwezo wake wa kuongoza
eneo la kiungo na mchango wake katika upande wa ulinzi na uanzishaji wa
mashambulizi.
Rodri alikuwa Manchester City kwa misimu saba, na
miongoni mwa mafanikio yake makubwa ni kushinda UEFA Champions League
2023 pamoja na mataji manne ya Premier League.
0 Comments