Msemaji wa
Klabu ya Yanga, Ally Kamwe amesema hakuna sababu ya Mashabiki kuwa na
hofu kuhusu taarifa zinazosambaa zikidai kuwa Klabu hiyo imefungiwa na
FIFA.
Akizungumza kuelekea Maadhimisho ya Yanga Day, Kamwe
amesema Viongozi wa Yanga wamechoshwa na mada hiyo kwa kuwa taratibu
zote za usajili zinafanyika kupitia mfumo rasmi unaosimamiwa na mamlaka
husika.
“Kuna vitu hata sisi tumechoka kuvielezea, hizi transfer
zote zinafanyika katika mfumo wa portal na TFF wanafuatilia na wanajua,
hivyo waulize TFF kwamba Yanga wamezuiwa,” amesema Kamwe.
Kauli
hiyo imekuja wakati kukiwa na mijadala kuhusu taarifa za kufungiwa kwa
Yanga na FIFA, huku Klabu ikiendelea na maandalizi ya Yanga Day, tukio
la kila mwaka linalowakutanisha Mashabiki kwa ajili ya utambulisho wa
kikosi, burudani mbalimbali na maandalizi ya msimu mpya wa mashindano.
0 Comments