ACT WAZALENDO WAMTAKA WAZIRI KIJAJI AJIUZURU

 Chama cha ACT Wazalendo kimemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, kujiuzulu kufuatia kifo cha kijana Seif Mussa, anayedaiwa kuuawa baada ya kukamatwa na askari wa Hifadhi ya Ngorongoro.

GUSA HAPA,REJESHA HESHIMA CHUMBANI NA KAMA UNAHITAJI AJIRA SASA  

Katika taarifa iliyotolewa Agosti 14, 2026 na Waziri Kivuli wa Maliasili, Utalii, Utamaduni na Michezo wa chama hicho, Emmanuel Ntobi, ACT Wazalendo kimesema kinashutumu vikali matukio ya mauaji yanayodaiwa kufanywa na askari wa hifadhi mbalimbali nchini, kikisema vitendo hivyo vinakiuka haki za binadamu na utawala wa sheria.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tukio la Agosti 12, 2026 katika Hifadhi ya Ngorongoro ni sehemu ya matukio mengi ya ukatili yanayodaiwa kufanywa na askari wa hifadhi dhidi ya raia bila hatua za dhati za uwajibikaji.

ACT Wazalendo imedai kuwa Seif Mussa, mwenye umri wa miaka 25, alikamatwa pamoja na vijana wengine wawili, Salimu Haji na Abdallah Nuru, ambao walipotea njia na kuingia katika eneo la hifadhi. Chama hicho kimesema vijana hao walipigwa na kuteswa, huku Seif akifariki kutokana na majeraha aliyopata.

Chama hicho kimesema kukamatwa kwa askari hao pekee hakutoshi, kikimtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, pamoja na Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Abdul Razaq Badru, kuchukua hatua za kisera na kiutendaji kutokana na matukio hayo.

Post a Comment

0 Comments