BEI MPYA YA MAFUTA KENYA TISHIO,TANZANIA YAONGOZA KWA UNAFUU

 TANZANIA imeendelea kuwa na bei nafuu ya mafuta ikilinganishwa na Kenya, baada ya mamlaka ya nishati ya Kenya, EPRA, kutangaza bei mpya zitakazoanza kutumika usiku wa leo, ambapo dizeli jijini Nairobi itauzwa KSh 217.86 sawa na takribani Sh 4,474 za Tanzania kwa lita, huku petroli ikiendelea kuwa KSh 214.03 sawa na takribani Sh 4,394 kwa lita.

TANGAZA NASI BIASHARA YAKO UFIKIE MAELFU YA WATEJA PIGA SASA 06544148094.

Bei hizo mpya zinakuja baada ya EPRA kupunguza dizeli kwa KSh 5 kwa lita, lakini hata baada ya punguzo hilo, mafuta nchini Kenya yanaendelea kuwa ghali zaidi ukilinganisha na bei za Agosti nchini Tanzania.


Kwa mujibu wa bei kikomo ziliotangazwa na EWURA na kuanza kutumika Agosti 5, 2026, jijini Dar es Salaam petroli inauzwa Sh 3,898 kwa lita, huku dizeli ikiwa Sh 3,978 kwa lita. EWURA huchapisha bei kikomo za mafuta kila mwezi kwa maeneo mbalimbali nchini.

Kwa ulinganisho wa Nairobi na Dar es Salaam, dizeli nchini Kenya ni ghali kwa takribani Sh 496 kwa kila lita, wakati petroli pia ni ghali kwa takribani Sh 496 kwa lita.

EPRA imeeleza kuwa punguzo la dizeli limetokana na gharama ya kuagiza bidhaa hiyo kushuka kwa asilimia 13.08, huku gharama ya mafuta ya taa ikishuka kwa asilimia 11.01.

Kinyume chake, gharama ya kuagiza Super Petrol ilipanda kwa asilimia 6.99, lakini bei yake haikupandishwa kutokana na hatua za Serikali ya Kenya za kutuliza bei.

Serikali ya Kenya imetumia takribani KSh 938 milioni kusaidia kuzuia ongezeko la bei za petroli na mafuta ya taa. Hata hivyo, ulinganisho wa bei mpya unaendelea kuipa Tanzania nafasi nzuri zaidi kwa unafuu wa bei za petroli na dizeli kati ya nchi hizo mbili, jambo lenye umuhimu mkubwa kwa gharama za usafirishaji, uzalishaji na maisha ya kila siku.

Post a Comment

0 Comments