Klabu ya
Wydad Athletic Club imekanusha taarifa iliyotolewa na Simba SC kuhusu
kuendelea kwa mchezaji Suleiman Mwalimu kuwa sehemu ya kikosi chake.
Kupitia taarifa rasmi, Wydad imesema maelezo yaliyotolewa hayalingani na
hali halisi ya kimkataba ya mchezaji huyo.
Wydad imeeleza kuwa
haijasaini mkataba wa mkopo wala makubaliano yoyote ya uhamisho wa muda
na Simba kuhusu Suleiman Mwalimu. Aidha, klabu hiyo imesisitiza kuwa
mchezaji huyo bado ana mkataba halali na Wydad na yupo ndani ya mipango
ya kiufundi ya timu.
Klabu hiyo imeongeza kuwa itachukua hatua
zote stahiki kulinda maslahi yake, huku ikiwataka mashabiki na vyombo
vya habari kutegemea taarifa zinazotolewa kupitia vyanzo rasmi vya Wydad
na kuepuka kusambaza taarifa ambazo hazijathibitishwa.
0 Comments