Mashirika
ya ndege ya Ulaya yameendelea kusitisha au kubadili njia za safari zake
katika baadhi ya maeneo ya Mashariki ya Kati baada ya mamlaka ya
usalama wa anga kuongeza tahadhari kutokana na hatari ya mashambulizi
mapya kati ya Marekani na Iran.
Uamuzi huo umetolewa na Wakala wa
Usalama wa Usafiri wa Anga wa Umoja wa Ulaya (EASA), ambao umeelekeza
waendeshaji wa ndege kuepuka kutumia anga la Iran, Iraq na Lebanon hadi
Agosti 31, 2026.
Katika taarifa yake ya Jumatano Julai 8, 2026,
EASA imeeleza hatua hiyo imechukuliwa kutokana na hali ya usalama
kutetereka tena baada ya mashambulizi kuendelea katika ukanda huo, licha
ya kuwepo kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani na
Iran.
Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, tathmini yake imehofia
uwezekano wa kuendelea kwa mashambulizi ya kijeshi endapo makubaliano
yaliyopo yataanguka.
Mvutano huo umeendelea baada ya Iran na
Marekani kushambuliana katika siku za karibuni, hatua iliyoongeza hofu
kwa sekta ya usafiri wa anga kutokana na uwepo wa maeneo yenye hatari
karibu na njia muhimu za ndege.
0 Comments