TANZANIA NA AFRIKA YA KUSINI KUSHIRIKIANA KUONDOSHA UPOTEVU WA MAJI

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) ametembela jiji la Pretoria mji wa shughuli za serikali nchini Afrika ya Kusini katika makao makuu ya Wizara ya Maji na Usafi wa Mazingira na kushiriki kikao kazi kilicholenga kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala mbalimbali yanayohusiana na utoaji wa huduma ya maji katika jamii.

Katika kikao ujumbe wa nchi zote umejadili teknolojia mbalimbali zinazohusiana na Sekta ya Maji na haswa teknolojia ya kuondosha upotevu wa maji.

Kikao kimewahusisha Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Bw. James G. Bwana, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri na wataalamu kutoka Wizara ya Maji.


 

Post a Comment

0 Comments