Kiungo
mshambuliaji wa Simba, Elie Mpanzu (Kibisawala) amefunguka sababu
zilizompelekea kusaini kandarasi jipya ndani ya Simba siku litakalomweka
klabuni hapo hadi mwaka 2028.
Kupitia ujumbe wenye hisia, Mpanzu
amekiri kuwa mapenzi ya mashabiki wa Simba ndiyo yaliyomfanya akatae
ofa nyingine na kuchagua kubaki nyumbani.
"Nikiwa na machozi
machoni mwangu ninawaandikia, wapenzi mashabiki wa Simba. Ninyi ndio
wafuasi bora zaidi ambao nimewahi kukutana nao. Nataka kuwashukuru
kutoka moyoni mwangu kwa msaada wenu usioyumba, licha ya nyakati ngumu
ambazo nimepitia. Mmekuwa mkiniamini kila wakati"
"Kutokana na
ushauri wenu kwamba ninaanza kurudi kwenye mstari ndiyo maana nimeamua
kutowasaliti na kuendelea na klabu. Ninawapenda nyote sana na
ninawaahidi mambo mema katika siku zijazo.
0 Comments