Tanzania imeingia hatua muhimu ya kuimarisha biashara na Marekani baada ya Serikali na Panda Hill Tanzania Limited kusaini mkataba wa makubaliano ya kuendeleza Mradi wa Niobium wa Panda Hill, hatua inayolenga kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha uzalishaji na usindikaji wa madini mkakati.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde alisema
mradi huo ni wa uzalishaji wa madini adimu ambayo hayapatikani kila
mahali duniani, na kwamba Tanzania inalenga kuchukua nafasi ya kipekee
katika soko la kimataifa la niobium kupitia mradi huo. Alisema soko la
dunia kwa sasa linatawaliwa na wazalishaji wachache wakubwa, na Panda
Hill itaiweka Tanzania kwenye ramani ya wazalishaji wakuu duniani.
Mheshimiwa
Mavunde alieleza kuwa mzalishaji mkubwa duniani yupo Brazil na
huzalisha takriban asilimia 80 ya mahitaji ya dunia, mzalishaji wa pili
naye yupo Brazil na huzalisha takriban asilimia 11, huku Canada
ikichangia takriban asilimia 6. Kupitia Panda Hill, alisema Tanzania
inalenga kuwa mzalishaji wa nne duniani kwa kuchangia takriban asilimia 4
ya mahitaji ya dunia, na uzalishaji unaolengwa kufikia takriban tani
100,000 kwa mwaka.
Katika kusisitiza mwelekeo wa Serikali, Waziri
Mavunde alisema dira ya maendeleo ya 2025-2050 na maelekezo ya Rais
Dkt. Samia Suluhu Hassan yanalenga kuhakikisha madini yanaongezewa
thamani hapa hapa nchini ili manufaa yawe makubwa kwa wananchi. Alisema
Tanzania inaenda zaidi ya uchimbaji wa kawaida kwa kujenga uwezo wa
ndani wa kuchakata na kuzalisha bidhaa za viwandani zenye thamani kubwa.
Mradi huo unahusisha niobium, madini ya kimkakati inayotumika kuongeza uimara wa chuma na kutengeneza aloi za utendaji.

.jpeg)





0 Comments