Mbeto Awataka Watanzania Kuyajua Yaliopo Duniani


Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi  kimesema kwa kile kinachopitiwa na Tanzania wakati   huu   hakikuanza   jana ,juzi au Mwezi uliopita bali ni mapambano  ya kiuchumi baada ya Ardhi  yake kugundulika Madini adimu duniani.
 

CCM kimesema huenda wakajitokeza maadui zaidi   watakaotumiwa kama njia ya kufanikisha  mkakati wa kuhatarishaa Amani endapo Watanzania watagawanyika. 

Katibu  wa Kamati Maalum  ya NEC  Zanzibar  , Idara ya Itikadi  , Uenezi na Mafunzo   ,Khamis  Mbeto  Khamis  ameeleza ameyaasa Mataifa  makubwa yaache kutoa visingizio vya kudhoofu kwa domokrasia au kutaja  chaguzi kuu hazikuwa huru.

Mbeto  alisema Duniani kumeibuka Vita ya Kiuchumi iliojaa hila na ghilba  zitokanazo  na uchu wa  kuhodhi Madini adim yanayohitajiwa kwa Maendeleo ya Mataifa makubwa.

Alisesma  hadithi au simulizi za  kuipa majina mabaya Tanzania na vitisho yabis ,  zilianza kwa kudai  kuna uongozi wa kidikteta  , ukandamizaji haki , demokrasia , Uhuru wa vyombo vya habari na kilichoitwa  kifo cha Upinzani.

" Hizi zote ni hadithi za ubabaifu .Miradi   miwili ya Uranium ya Mkuju na
 Liganga  imefumua  joto la taharuki  duniani. Wakati  Mkuju si mgodi tu wa Uranium bali pia ni  mojawapo ya maeneo muhimu Duniani" Alisema Mbeto 

Alisema hatua ya Shirika la Nyuklia la Urusi  kuchukua  Mradi wa Nyuklia , ndio  mwanzo wa kuzuka fitna nyeusi  baada ya Tanzania na Urusi kuzindua Kiwanda cha majaribio cha usindikaji wa Uranium Mkuju.

Alisema  kwa  Mradi wa Lindi Liganga ,
Kampuni za  Magharibi toka Mwaka 2018–2023  zilijadiliana bila mafanikio huku China ,  Falme za Kiarabu  na Gazprom ya Urusi, zikionyesha nia ya kuanza kushiriki.

 "Taswira iliopo ni Uranium kwenda  Urusi Gesi itahodhiwa na  China , Nchi za  Gulf , Urusi  huku nchi za Magharibi zikitaka kujua endapo  hakutakuwa na mabadiliko yoyote " Alieleza

Mbeto  alisema hapo ndipo ilipoanza  vita ya kidijitali kwani kama inavyojulikana siku hizi   vita haipiganwi kwa bunduki bali kwa matumizi ya  mitandao ya kijamii .

"Tanzania  haitapuuza msimamo  wake  wa kujadiliana na  kiungwana  ili kufikia makubaliano ya kiungwana. Vitisho na  propaganda uchwara lazima zikomeshwe . Madai ya udhaifu wa  demokrasia ,  chaguzi  kutokuwa huru au ukandamizaji wa aina yoyote zikome "Alieleza 

Hata hivyo, Katibu huyo Mwenezi alisema Tanzania  haitabaki  peke  yake,  badala yake itashirikiana na Dunia ili  kulinda  Utu na maslahi  yake na kuyapa indhar  Mataifa kadhaa yaache   kutumia  mradi wa udini, ukabila na kupandikiza  mamluki.


Post a Comment

0 Comments