MALISA AKIRI WANAOCHOCHEA VURUGU SIO WATANZANIA-MCHANGE

Suala la Thadei Kweka lafichua hatari ya watu walioukana uraia kuingilia masuala ya ndani ya Taifa.

Taarifa iliyotolewa na Malisa Godlisten akidhani analichafua jeshi la polisi kumkata Mtanzania aliyeukana utanzania na kuwa mmarekani Thadei Kweka imeweka wazi ukweli mzito unaopaswa kuangaliwa kwa jicho la Taifa kuwa watu wanaohamasisha vurugu,uchochezi na uvunjifu wa amani si Watanzania, na hata watanzania wachache hawaishi Tanzania kama inavyozidi kubainika 

Kwa mujibu wa taarifa ya Malisa , Thadei Kweka anayetajwa katika sakata hilo sio raia wa Tanzania, bali ni raia wa Marekani aliyeukana uraia wa Tanzania, na aliingia nchini kwa Tourist Visa ya muda wa siku 90. 

Huu ni uthibitisho wa wazi kwamba mhusika hakuwa nchini kama Mtanzania, bali kama mgeni ambaye kipindi akiwa marekani alikuwa anatukana serikali, anashawishi vurugu na uchochezi huku watanzania hasa vijana wakijua ni mwenzao .

Kukana Uraia ni Kukana Taifa

Ifahamike kuwa Uraia wa nchi si hati ya kusafiria pekee, bali ni Kiapo cha utii kwa Taifa, Ahadi ya kulinda amani na mshikamano na Msingi wa mapenzi ya dhati kwa nchi

Mtu anapoukana uraia wa Tanzania, kwa mantiki hiyo anaukana Utii kwa mamlaka ya nchi, Wajibu wa kulinda amani ya Taifa, Maadili na misingi ya utaifa na kupoteza sifa na hazi zote za watanzania 

Haiwezekani mtu aliyelikataa Taifa abaki na madai ya kulipangia wake, hususan kwa njia zinazohatarisha amani na usalama wa nchi.

Taarifa ya Malisa inaonesha pia kuwa hata taratibu za kidiplomasia zilihusishwa, ikiwemo kuwasiliana na ubalozi wa Marekani, jambo linalozidi kuthibitisha kuwa anayezungumziwa hakuwa Mtanzania, bali raia wa nchi nyingine.

Watanzania wa Kweli Wanachagua Amani

Historia na uhalisia wa Tanzania unaonesha kuwa Watanzania wanapotofautiana, hutumia njia za kikatiba, Wanapodai haki, hutanguliza amani na utulivu, Hawachochei machafuko yanayohatarisha maisha, mali na mustakabali wa Taifa

Ni dhahiri kuwa vurugu nyingi hazichochewi na Watanzania halisi, bali na watu waliokata mizizi yao ya utaifa, au wasiokuwa na dhamira ya kweli kwa mustakabali wa nchi.

Kwa msingi wa taarifa ya Malisa Godlisten, hoja ni wazi kuwa watu waliokata tamaa, wakaukana uraia wa Tanzania, hawawezi kuwa na mapenzi ya Taifa.

Na pale watu wa aina hiyo wanapojaribu kuingilia masuala ya ndani ya nchi, Taifa lina wajibu wa kusimama imara kulinda amani, mamlaka na heshima ya Tanzania.

Habibu Mchange
Mwenyekiti-MECIRA

Post a Comment

0 Comments