TAKUKURU SPORTS CLUB YAKABIDHI MAKOMBE YA USHINDI KWA MKURUGENZI MKUU

Klabu ya Michezo ya TAKUKURU imemaliza mashindano ya michezo ya 39 ya SHIMIWI kwa kuibuka 'Mshindi wa Jumla' katika Michezo ya 39 ya SHIMIWI na kukabidhi kwa Mkurugenzi Mkuu, vikombe na medali zilizopatikana.

Akipokea zawadi hizo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu katika hafla iliyofanyika Septemba 18, 2025 TAKUKURU Makao Makuu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bibi Neema Mpembe Mwakalyelye, amewapongeza wanamichezo kwa kufanya vizuri katika mashindano na kupata ushindi mkubwa uliosababisha TAKUKURU kupata ushindi wa Jumla wa Mashindano ya SHIMIWI mwaka 2025.

Bibi Neema alisema kuwa matokeo mazuri na ushindi uliopatikana umeitangaza vema TAKUKURU kwa sababu mara zote timu zilipopata ushindi TAKUKURU ilitangazwa katika vyombo mbalimbali vya Habari.



Post a Comment

0 Comments