VIDEO ILIYOWAKERA WENGI MITANDAONI,POLISI WATOA UKWELI WOTE KUHUSU TUKIO HILO

Jeshi la Polisi nchini limetolea ufafanuzi picha mjongeo inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikionesha Dereva wa Pikipiki akizozana na Askari Polisi huku askari hao wakijitahidi kuyaondoa barabarani magunia ya alizeti aliyokuwa amebeba dereva huyo kwenye pikipiki.

Tukio hilo lilitokea Julai 30,2026 Wilaya ya Bariadi Mkoa wa Simiyu.

Askari hao walikuwa wanapitisha msafara wa Mwenge wa Uhuru ndipo Dereva huyo wa pikipiki alisimamishwa kwa ajili ya usalama wake na wa watu wengine làkini alikaidi ndipo ikabidi Askari wamzuie na matokeo yake pikipiki ikadondoka.

Polisi wamesema tukio hilo lilianza kushughulikiwa na kuchukuwa hatua kuanzia hiyo Julai 30,2026 ikiwa ni pamoja na kupata maelezo sahihi ya walioshuhudia kilichotokea toka mwanzo.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa wito kwa kila mmoja kutii sheria na kufuata maelekezo ya kiusalama yanayotolewa kwa ajili ya usalama wetu ili kuepuka madhara na migongano isiyo ya lazima.

 

Post a Comment

0 Comments