TAHARUKI MWENGE! BOKSI LA AJABU LILILOTELEKEZWA LAZUA HOFU, POLISI WALICHUKUA KWA UCHUNGUZI

Boksi ambalo bado halijafahamika lina nini ndani yake limekutwa Kituo cha Mabasi cha kwenda Tegeta maeneo ya Mwenge, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa mtaa wa Mlalakuwa, Suleiman Masare amesema kuwa boksi hilo lilitelekezwa tangu jioni ya jana Jumatano Agosti 5,2026.

Masare amesema boksi hilo limezua taharuki kwa wananchi, huku Jeshi la Polisi likianza taratibu za kulikagua na kulifungua ili kubaini kilichomo ndani na kuondoa hofu iliyojitokeza.

Jeshi la Polisi limechukua boksi lililokuwa limetelekezwa eneo la Mwenge, Dar es Salaam kwa ajili ya uchunguzi.

Boksi hilo limepelekwa Kituo cha Polisi Mabatini, Kijitonyama, ambako taratibu za uchunguzi zinaendelea.

Jeshi la Polisi limesema taarifa kamili kuhusu kilichomo ndani ya boksi hilo itatolewa kwa umma baada ya uchunguzi na kulifungua kukamilika.

Post a Comment

0 Comments