Jeshi la
Polisi Mkoa wa Rukwa limewafikisha mahakamani watu wawili kwa tuhuma za
mauaji ya Ferdinand Kefa Msakuzi (50), mkazi wa Majengo, Wilaya ya
Sumbawanga.
Watuhumiwa hao ni Michael John Bubinza, aliyekuwa
askari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa, na Spiliano Mmanyo Pascal,
dereva wa bodaboda, wote wakiwa wakazi wa Sumbawanga.
Tukio hilo
la mauaji liligundulika tarehe 28 Julai 2026, majira ya saa 6:00
mchana, katika Kijiji cha Kisumba, Wilaya ya Sumbawanga, ambapo mwili wa
marehemu ulikutwa umetupwa vichakani.
Baada ya uchunguzi wa
awali kukamilika, tarehe 19 Agosti 2026, watuhumiwa hao walifikishwa
katika Mahakama ya Wilaya ya Sumbawanga, ambako walisomewa shtaka la
mauaji.
0 Comments