MWANAFUNZI AUWAUA WAZEE NA WALIMU KWA RISASI

 Watu kadhaa wameuawa na zaidi ya 20 wamejeruhiwa katika shambulizi la risasi katika shule moja kaskazini mwa Bangkok, nchini Thailand.

Vyombo vya habari nchini humo vikinukuu mamlaka, vimesema walimu watano ni miongoni mwa waliouawa katika shambulizi hilo lililotokea leo asubuhi muda mfupi baada ya saa 10:00 kwa saa za huko (saa 03:00 GMT) katika Shule ya Debsirin Nonthaburi, jimboni Nonthaburi nchini Thailand.

Polisi wanasema mshukiwa, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tisa, mwenye umri wa miaka 14 alipatikana amekufa darasani, akiaminika kujipiga risasi baada ya shambulizi huku risasi nyingi zikipatikana kwenye begi lake.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa kabla ya kwenda shuleni, kijana huyo huenda aliwaua babu na bibi yake kwa kutumia bunduki ya babu yake.
Mamlaka pia zinachunguza madai kwamba mwanafunzi huyo alikuwa akifanyiwa vitendo vya uonevu shuleni.

Tukio hili la ufyatuaji risasi linafuatia tukio jingine katika shule iliyo kusini mwa Thailand mwezi Februari.

Post a Comment

0 Comments