Moto ambao
chanzo chake bado hakijajulikana umeteketeza nyumba ya wapangaji yenye
vyumba 17 katika Mtaa wa Maisaka, Wilayani Babati mkoani Manyara, na
kuacha wananchi kadhaa bila makazi baada ya kushindwa kuokoa mali zao.
GUSA HAPA,REJESHA HESHIMA YAKO CHUMBANI SASA
Mashuhuda
na waathirika wa tukio hilo, akiwemo Christina Patrice, Ester Alex, na
John Kelvin, wameeleza kuwa moto huo ulianza usiku wa kuamkia leo baada
ya kusikia mlipuko wa ghafla uliosababisha moto kusambaa kwa kasi kwenye
vyumba hivyo.
Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa Jeshi la Zimamoto
na Uokoaji Mkoa wa Manyara, Emmanuel Kibona, amethibitisha kuwa askari
waliwahi eneo la tukio na kufanikiwa kudhibiti moto huo kwa asilimia
100, huku kukiwa hakuna vifo wala majeruhi walioripotiwa.
Hata
hivyo, kutokana na kupoteza mali na makazi yao yote, waathirika wa janga
hilo wametoa kilio na wito kwa Watanzania na wadau mbalimbali
kuwasaidia misaada ya kibinadamu ili kuweza kujikimu.
0 Comments