Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, amemfuta kazi Waziri wa Ulinzi na kufanya mabadiliko kadhaa katika ngazi za juu za jeshi, kulingana na vyombo vya habari vya serikali.
Shirika la habari la KCNA limesema uamuzi huo ulifikiwa katika mkutano ulioongozwa na Kim Jong Un, ambapo viongozi walijadili kile kilichoelezwa kuwa mpango wa marekebisho ya muundo wa jeshi.Kwa mujibu wa KCNA, Noh Kwang-chul ameondolewa katika wadhifa wa Waziri wa Ulinzi na kushushwa cheo kuwa naibu mkuu wa kwanza wa Idara ya Viwanda vya Silaha ndani ya chama tawala.
Nafasi hiyo sasa itashikiliwa na Kim Song-gi, ambaye alikuwa mkuu wa Idara Kuu ya Siasa ya Jeshi la Watu wa Korea.
Katika
mabadiliko hayo, mshauri wa masuala ya ulinzi wa Kim Jong Un, Pak
Jong-chun, ameteuliwa kuwa makamu mwenyekiti wa Tume Kuu ya Kijeshi
pamoja na kuwa mjumbe wa Politburo ya Chama cha Wafanyakazi wa Korea.
Vyombo
vya habari vya serikali havikutoa sababu za mabadiliko hayo. Hata
hivyo, hatua hiyo imekuja wakati Korea Kaskazini ikiendelea kuimarisha
uwezo wake wa kijeshi na kuimarisha ushirikiano wa kiulinzi na Urusi,
huku mvutano katika Rasi ya Korea ukiendelea.

0 Comments