BODI YA LIGI:KULALAMIKIA FVS SIO KAZI YA WACHEZAJI

Kamati ya bodi ya ligi pia imezikumbusha timu zote kuzingatia kikamilifu kanuni ya 20 inayohusu matumizi ya Teknolojia ya Football Video Support System (FVS), ikisisitiza kuwa mchezaji haruhusiwi kumlalamikia au kumshinikiza mwamuzi kuomba marejeo ya matukio.

 GUSA HAPA,UREJESHE HESHIMA CHUMANI NA TIBA LISHE

Kwa mujibu wa Kanuni ya 20(4), Kocha Mkuu au kiongozi mwingine wa juu kwenye benchi la ufundi ndiye mwenye mamlaka ya kuwasilisha ombi la marejeo ya tukio katika mfumo wa FVS, kupitia Mwamuzi wa Akiba. 


Kanuni hiyo pia inaelekeza kuwa iwapo mchezaji ataona tukio linahitaji marejeo ya FVS, anatakiwa kumjulisha kocha mkuu au kiongozi wa benchi la ufundi kwa ishara, ili kiongozi huyo awasilishe ombi hilo.

Kamati imeonya kuwa ni marufuku kwa mchezaji kumlalamikia au kumshinikiza mwamuzi moja kwa moja kwa lengo la kuomba marejeo ya FVS. Mchezaji atakayekiuka masharti hayo ataadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62.

Kiongozi au Kocha pekee anatosha kuomba marejeo ya matukio kupitia FVS ?

Post a Comment

0 Comments