Jeshi la
Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamshikilia John Daud (42), mkazi wa Mtaa
wa Lenguwa wilayani Moshi, kwa tuhuma za kuchoma moto jengo la zamani la
Mahakama ya Mwanzo ambalo halitumiki kwa sasa.
Tukio hilo
lilitokea Agosti 24, 2026 asubuhi na kusababisha vyumba vinne pamoja na
nyaraka zilizokuwemo ndani kuteketea, kabla ya Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji kwa kushirikiana na wananchi kufanikiwa kuuzima bila kuleta
madhara kwa binadamu huku thamani ya mali zilizoharibika ikiwa bado
haijafahamika.
Kufuatia tukio hilo, polisi walianzisha msako
mkali na kufanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa huyo Agosti 25, 2026 akiwa
kwenye hafla ya Maulidi.
Jeshi hilo limeeleza kuwa uchunguzi wa
kina unaendelea kwa ushirikiano na vyombo vingine vya kiusalama, na mara
utakapokamilika, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani ili kujibu mashtaka
yanayomkabili.
0 Comments