Katibu
wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani
Kihongosi, amewataka Watanzania kutowasikiliza wanasiasa wanaotumia
majukwaa ya siasa kutoa matamshi ya kubeza na kupunguza thamani ya
miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.
Kihongosi ametoa
wito huo Mkoani Iringa wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi akiwa
katika ziara yake ya kikazi ya kuimarisha chama na kukagua miradi ya
maendeleo.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.
Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi katika elimu, afya, maji na
miundombinu, na matokeo yake yanaonekana kila mkoa lakini kuna baadhi ya
wanasia wamekuwa wakitumia baadhi ya madhaifu machache kuwaaminisha
kuwa hakuna kitu kilichofanywa na serikali.
0 Comments