Simba SC
imetwaa tuzo ya Klabu Bora ya Wanaume wa mwaka katika Tuzo za Baraza la
Michezo la Taifa (BMT) 2025 zilizofanyika Jijini Dar es salaam huku
mafanikio hayo yakidhihirisha mwendelezo wa ubora wa Klabu hiyo katika
mashindano mbalimbali ya ndani na Kimataifa kwa mwaka 2025.
Tuzo
hiyo imetolewa Mei 9, 2026 katika Ukumbi wa The Super Dome, Masaki
Jijini Dar es salaam ambapo imekabidhiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, na kupokewa na Afisa
Mtendaji Mkuu wa Simba SC, Zubeda Sakuru mbele ya Wadau mbalimbali wa
michezo Nchini.
Katika tuzo za Wanamichezo binafsi, Mwanariadha
Alphonce Simbu ametwaa tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Kiume wa mwaka huku
Stumai Abdallah wa JKT Queens na Timu ya Taifa ya Wanawake akitwaa tuzo
ya Mwanamichezo Bora wa Kike wa mwaka kutokana na mafanikio yao katika
mashindano mbalimbali ya Kimataifa.
Kwa upande wa Vijana, Raymond
Francis ametangazwa kuwa Mwanamichezo Bora Kijana wa Kiume wa mwaka
huku Rose Kataboy akitwaa tuzo ya Mwanamichezo Bora Kijana wa Kike baada
ya kuonyesha kiwango bora katika michezo yao kwa mwaka 2025.
Mbali
na Wanamichezo, tuzo nyingine zilizotolewa ni pamoja na Kocha Bora wa
Kiume aliyekwenda kwa Anthony Mwingereza, Kocha Bora wa Kike
aliyotwaliwa na Esther Chabruma, Mwamuzi Bora wa Kiume aliyeshinda
Shabani Mahobonya, Mwamuzi Bora wa Kike aliyokwenda kwa Dariso Mwidadi
pamoja na tuzo za Wanahabari wa michezo zilizotwaliwa na Fatma Chikawe
na Khalid Msabaha
0 Comments