YANGA MNAIWEZA SASA,PRISONS WAPIGIKA TENA

 Na Ally Mandai.

Wananchi, Young Africans SC wamechomoza na ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Wajelajela, Tanzania Prisons katika dimba la KMC Complex na kuendelea kujitanua zaidi kileleni mwa msimamo wa Ligi kuu bara.

Wananchi wamefikisha alama 41 baada ya mechi 17 na kusogea mpaka alama 7 mbele ya mahasimu wao, Simba Sc waliopo nafasi ya pili ingawa Yanga SC imecheza mechi mbili zaidi.

FT: Yanga SC 3-0 TZ Prisons
⚽ 50’ Okello (🅰️ Mwenda
⚽ 68’ Mudathir (🅰️ Okello)
⚽ 86’ Pacome (🅰️ Abuya).

TANGAZA NASI BIASHARA YAKO KWA ELFU 20,000/= TU UWAFIKIE MAMILIONI YA WATEJA PIGA 0654414804.


 

Post a Comment

0 Comments