Mechi ya
fainali ya Kombe la Muungano 2026 kati ya Wananchi, Young Africans SC
dhidi ya Wekundu, Msimbazi, Simba SC itaamuliwa na mwamuzi Dickens
Mimisa Nyagrowa kutoka Kenya ambaye atakuwa mwamuzi wa kati.
Mwamuzi
msaidizi namba moja kwenye mechi hiyo ya Dabi ya Kariakoo ni Ali Mbwana
kutoka Zanzibar huku mwamuzi msaidizi namba 2 akiwa Yusuph Shombe
kutoka Zanzibar wakati mwamuzi wa akiba (4th offical) akiwa ni Is’haka
Mwalile.
Mchezo huo utakaowakutanisha mahasimu hao wakubwa Nchini
utapigwa leo Aprili 29, 2026 katika dimba la New Amaan Complex,
Zanzibar majira ya saa 2:15 usiku.
0 Comments