LATRA YAONYA DHIDI YA ONGEZEKO LA NAULI KIHOLELA

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini, LATRA, imeonya watoa huduma za usafiri nchini kuacha mara moja kupandisha nauli kiholela bila kufuata taratibu za kisheria.

Onyo hilo linakuja wakati baadhi ya waendeshaji wa mabasi na daladala wakianza kuongeza nauli wakihofia kupanda kwa gharama za uendeshaji, hali inayowaathiri wananchi, hasa wa kipato cha chini na wanafunzi.

Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, Habib Suluo, alisema mamlaka hiyo inatambua changamoto za sekta hiyo, lakini mabadiliko ya nauli lazima yafanyike kwa kufuata sheria na kanuni zilizowekwa.

“Hatutaruhusu ongezeko holela la nauli. Lazima utaratibu ufuatwe ili kulinda maslahi ya wananchi,” alisema.

Alisema LATRA itaitisha kikao cha wadau Aprili 8 jijini Dar es Salaam kujadili hali hiyo na kupata suluhisho la pamoja.

Kwa mujibu wa sheria, nauli hupangwa na LATRA, kuidhinishwa na Bodi ya Wakurugenzi na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali kabla ya kuanza kutumika rasmi baada ya siku 14.


 

Post a Comment

0 Comments