Na Ally Mandai.
Chama
cha ACT Wazalendo kimefuatilia uwasilishwaji wa Taarifa ya Tume ya
Uchunguzi wa Mauaji ya Oktoba 2025 iliyowasilishwa leo. Chama kinasimama
imara katika msimamo wake wa kukataa kile kinachoitwa Tume ya Chande,
ambayo tangu mwanzo tulieleza kuwa haina uhuru na imeundwa kama chombo
cha kulinda wahusika badala ya kutoa haki. Msimamo wetu huo umethibitika
leo.
Ripoti iliyowasilishwa leo
na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mkuu Mstaafu Ndg. Mohamed. Chande
Othman kwa Rais Sania Suluhu Hassan ina hitimisho ambalo lilitarajiwa
kabisa kutokana na muundo wake, wajumbe wake na hadidu rejes za Tume
hiyo.
ACT Wazalendo tunaombeleza
kila maisha yaliyopolezwa na kila familia iliyopata madhila kufuatia
matukio ya tarehe 29 Oktoba na athari zake. Uponyaji wa kweli wa taifa
na maridhiano ya dhati yanaweza kupatikana tu kupitia uchunguzi huru, wa
kuaminika na ulio wazi.
Tumeshangazwa
kusikia kuwa baada ya Tume ya Jaji Chande, sasa kutaundwa Tume
nyingine. kufanya uchunguzi wa kijinai wa matukio yale yale. Hii ni
ujanja ujanja mwingine wa kupoteza muda mwingine na kutafuna fedha za
walipa kodi. Watanzania hawawezi kukubali ulaghai na ujanja ujanja wa
aina hii
ACT Wazalendo tunarudia
wito wetu wa kuundwa kwa uchunguzi huru wa kimataifa chini ya taasisi
zenye kuaminika kama Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika au SADC
Hii
ni kauli yetu ya awali. Msimamo wa kina zaidi utakaoangazia maeneo yote
utatolewa baada ya kikao cha Kamati ya Uongozi ya Chama Taifa
itakayoketi hivi karibuni katika kipindi cha wiki moja.
Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinarejea msimamo wake wa awali
wa tarehe 19 Novemba 2025 kutotambua mchakato mzima wa Tume iliyoundwa
na Samia Suluhu Hassan, na kinapinga kwa ujumla wake ripoti
iliyowasilishwa leo tarehe 23 April 2026 na Tume hiyo chini ya Jaji
Mohamed Chande Othman.
CHADEMA
inasisitiza kuwa, kwa mujibu wa kauli ya wazi ya Samia Suluhu Hassan
mwenyewe, ripoti hiyo ni yake binafsi. Hivyo, haiwezi kuchukuliwa kama
nyaraka huru yenye kuakisi ukweli au haki kwa waathirika wa matukio
yaliyoripotiwa.




0 Comments