Rais wa
Uganda, Yoweri Museveni amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC), akipokea kijiti cha uongozi kutoka kwa
mtangulizi wake Rais wa Kenya, William Ruto.
Nafasi hiyo ya
Uenyekiti wa Museveni, imetangazwa leo Machi 7, 2026 Jijini Arusha
katika Mkutano wa Kawaida wa 25 wa wakuu wa nchi wa jumuiya hiyo
unaoendelea jijini humo.
Museveni anachukua nafasi hiyo, huku
akitarajiwa kuongoza ajenda za kuimarisha ushirikiano wa kikanda, kukuza
uchumi na maendeleo ya pamoja ya nchi wanachama wa EAC.
0 Comments