RAIS SAMIA ATOA PONGEZI KUBWA KWA WANAWAKE TANZANIA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

 Na Ally Mandai.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Dkt. Samia Suluhu Hassan leo ametoa salamu za heri na pongezi kwa wanawake wote nchini ikiwa ni sehemu ya kusheherekea siku ya kimataifa ya wanawake.

"Ninawapongeza na kuwatakia kheri wanawake wote katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake. Siku hii inatupa fursa ya kipekee ya kutambua, kujivunia na kusherehekea mafanikio tuliyopata, hasa katika elimu, afya, uchumi na uongozi".

"Siku hii inatukumbusha pia wajibu wetu wa msingi kwa waasisi wetu na kwa vizazi vya sasa na vijavyo; wa kuendelea kupanga na kutekeleza mipango ya kumwezesha mwanamke, ikiwa ni sehemu muhimu ya kazi ya kukomboa familia, jamii na Taifa kwa ujumla".


 

Post a Comment

0 Comments