CCM ITAENDELEA KUZUNGUMZA NA VYAMA,MAKUNDI YOTE KWA MASLAHI YA AMANI YA TANZANIA

 Na Mwandishi Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi   kimesema kimepokea taarifa  ya maendeleo ya mazungumzo  yanayotafuta Muafaka wa utatuzi wa  Kisiasa yenye lengo la  kuendeleza Serikali  ya Umoja  wa Kitaifa Zanzibar. 

Aidha,  CCM kimetaja  mazungumzo hayo kuwa bado  siri huku  yakisimamiwa na Marais  Wastaafu wa  Zanzibar , Dk Amani Abeid  Karume na Dk Ali  Mohamed  Shein. 

Hayo ameyaeleza  Katibu Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar, Cde: Khamis Mbeto Khamis,  Ofisini kwake wakati akitoa taarifa ya uwepo wa mazungumzo baina ya ACT na Wazalendo baada ya kukamilika kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu Taifa kilicho fanyika tarehe 19/2/2026 katika Afisi kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar, 

Mbeto  alisema Msingi wa mazungumzo hayo , umejiegemeza katika kuzipitia hitilafu,  dosari na kasoro  mbambali za Kisiasa na Kisheria ,  hatimae ziweze kurekebishwa .

Alisema pia katika Majadiliano hayo zitaangaliwa kasoro na dosari  endapo ni za kisheria ,  zitapelekwa katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar,  kufanyiwa Marekebisho ya kisheria kwa mujibu wa katiba ya zanzibar ya mwaka  1984.

"Kamati Maalum  ya NEC Zanzibar imepokea taarifa ya  kuendelea kwa mazumgumzo kati ya  CCM na ACT  . Agenda za mjadala huo  bado ni siri . Hatma ya mazumgumzo hayo ikifikiwa  itatangazwa  na pande zote mbili" Alisema Mbeto 

"Katika Majadiliano ikiwa kutaonekana haja ya kubadili jambo husika  kisheria , suala  hilo  litapelekwa Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Kwa mfano huwezi kuondosha 
Kura ya mapema bila kubadili sheria yake. "Alisema Mbeto 

Katibu  huyo Mwenezi  alisema ni majadiliano  yenye nia njema kwa mustakabali na ustawi wa Zanzibar na Wananchi wake .

"Wajumbe   Washiriki kwenye mazungumzo hayo watarudisha mrejesho kwa chama kilichowatuma. Hatua nyingine za Vikao vya juu vya  chama  chetu zitafuata na kutoa maamuzi yake   "Alisema Mbeto



Post a Comment

0 Comments