BANDARI DAR ES SALAAM YAJIVUNIA ONGEZEKO LA MELI KUBWA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyarara amesema kuwa serikali inaendelea kuwekeza kwenye bandari ya dar esalaam ikiwa ni kutokana na ongezeko la Meli kubwa kuingia katika bandari hiyo  hivyo  imesababisha shehena ya Mzigo kuongezeka huku wadau wa Bandari  wametakiwa kuchukua mizigo yao  kwa wakati ili kutoa fursa kwa  Mizigo mingine iweze  kuhudumiwa kwa wakati.

Akizungumza Jijini Daresalaam  kwenye kikao cha wadau wa Maboresho ya Bandari Katibu Mkuu wizara ya uchukuzi Profesa Godius kahyarara amewataka  wadau wa Bandari na Taasisi mbalimbali za Serikali na Sekta binafsi kushirikiana katika kutoa huduma  wakiwemo TRA, TASHICO,TTFCA, TBS , Wamiliki wa Maroli, Wizara ya mambo ya Ndani, TAMISEMI na Wizara ya Uchukuzi.

“Serikali inaendelea kuwekeza zaidi  katika bandari ya Dar es salaam kwa kuboresha na  kuongeza kina cha mlango wa bahari, ujenzi wa magati na ununuzi wa vifaa na kushirikisha sekta binafsi ambapo  imepelekea    kuongeza  shehena katika bandari ya Da er Salaam”alisema Kahyarara.

Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Dar es salaam Abed Gallus ameongeza kuwa kutokana na kuongezeka kwa shehena hasa Makasha (Conteina) Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari  (TPA) wanaendelea na upanuzi wa maeneo mengine kwa ajili ya kuhifadhia Makasha hayo. Pia  ICDs nyingi zimejaa hivyo mamlaka hiyo  inaongeza maeneo kama vile EPZA ili kuweka Makasha.

 Naye  Meneja wa Undeshaji  kutoka  Shirika la reli Tanzania (TRC )Focus Sahani amesema kwa sasa Serikali imenunua vichwa nane kwa ajili ya kupeleka Makasha katika Bandari Kavu ya kwala ambapo vichwa viwili tayari vimeanza kazi na vichwa sita vipo katika majaribio.



Post a Comment

0 Comments