𝐍𝐄𝐌𝐂 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐉𝐈𝐓𝐈𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐙𝐀 𝐌𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐈𝐖𝐀 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐊𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐔𝐍𝐙𝐀 𝐌𝐀𝐙𝐈𝐍𝐆𝐈𝐑𝐀

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, za kuhifadhi na kusimamia mazingira kwa kushiriki zoezi la upandaji miti katika kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa tarehe 27 Januari.

Katika kuadhimisha siku hiyo, Mheshimiwa Rais alipanda mti kama ishara ya kuhamasisha uhifadhi wa mazingira, ikiwa ni utekelezaji wa kaulimbiu isemayo “Uzalendo ni kutunza mazingira, shiriki kupanda miti.”

Kupitia kanda zake 13 nchini kote, NEMC imeshirikiana na wizara, taasisi za umma na binafsi, asasi za kiraia pamoja na kamati za mazingira kushiriki katika zoezi la upandaji miti katika maeneo mbalimbali yakiwemo shuleni, zahanati na katika masoko.

Akizungumza katika hafla hiyo, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mkurugenzi wa  Utawala na Fedha Bw. Dickson Mjinja alieleza umuhimu wa kupanda miti kama njia mojawapo ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi huku akisisitiza kuwa miti ina mchango mkubwa katika kuhifadhi ikolojia na kuboresha maisha ya binadamu.

Kwa upande wake, Meneja wa NEMC Kanda ya Ilala, Bi. Abella Muyungi, aliwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kusimamia na kuhifadhi mazingira nchini kwa vitendo, akisisitiza kuwa jukumu la uhifadhi wa mazingira ni la kila mmoja.

NEMC imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuunga mkono juhudi za Serikali za awamu ya sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kulinda na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

Zoezi la upandaji miti Kata ya Ilala viwanja vya msikate tamaa limeratibiwa na NEMC na Balozi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Grit Godfrey.







 

Post a Comment

0 Comments