Mkuu wa Jeshi
la Uganda, Muhoozi Kainerugaba, ametangaza nia ya kuwania Urais wa
Uganda mwaka 2031, akisema anaamini ataweza kushinda kwa asilimia 90
iwapo atapata msaada wa baba yake, Rais Yoweri Museveni.
Muhoozi,
mwenye umri wa miaka 52, ni mtoto wa Museveni ambaye amekuwa Rais wa
Uganda tangu mwaka 1986 ambapo amejulikana pia kwa kauli zenye utata
kwenye mitandao ya kijamii, ikiwemo vitisho dhidi ya kiongozi wa
upinzani Bobi Wine.
Katika ujumbe wake aliyo uchapisha katika
ukurasa wake kwenye mtandao wa X, Muhoozi amesema “Nitawania nafasi ya
juu zaidi nchini mwaka 2031, na tutashinda kwa neema ya Mwenyezi Mungu,”
Muhoozi aliwahi kutangaza nia ya kuwania Urais katika uchaguzi
wa Januari 2026, lakini baadaye alijiondoa na kumuunga mkono baba yake,
ambaye alichaguliwa tena licha ya upinzani na mashirika ya haki za
binadamu kukosoa hatua za serikali dhidi ya wapinzani.
0 Comments