ALIYEGONGA MTOTO AKIVUKA BARABARA AKAMATWA

 Jeshi la PolIsi mkoani Mwanza linamshikilia Mdamo Masalu Nyalwisila (40) dereva wa gari lenye namba za usajili T 885 ENK, aina ya Scania, mali ya kampuni ya Seedco Tanzania Limited, lililokuwa likitokea Mwanza mjini kuelekea Bariadi kwa kumgonga mtembea kwa miguu aliyekuwa anavuka barabara kutoka upande wa kulia mwa barabara kwenda upande wa kushoto mwa barabara, aitwaye Prosper Yusuph Msafiri, mwenye umri wa miaka 07, mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Wita na mkazi wa Kisesa,na kumsababishia kifo.

Baada ya ajali hiyo iliyotokea katika kata ya Kisesa, tarafa ya Sanjo, wilaya ya Magu, katika Barabara Kuu ya Mwanza-Musoma, wananchi waliokuwepo eneo hilo walifunga barabara hiyo na kuzuia shughuli za usafirishaji zisiendelee jambo lililosababisha adha kubwa eneo hilo.

licha ya viongozi mbalimbali wa Serikali kuwaomba wananchi wa eneo hilo kuwa watulivu wakati hatua za kisheria zitachukuliwa kwa dereva pamoja na kutekeleza ombi lao kuweka matuta ya barabarani eneo hilo, bado wananchi walikaidi na kuanza kurusha mawe jambo lililopelekea jeshi la polisi kulazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya watu waliokuwa wanarusha mawe na kufanya vurugu eneo hilo kwa ajili ya kurejesha amani eneo hilo.

Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva kushindwa kuchukua tahadhari katika maeneo yenye makazi ya watu.

Post a Comment

0 Comments