Na Ally Mandai.
Mtoto mwenye
umri wa miaka mitatu na miezi kumi wa jinsia ya kike aliyeripotiwa na
mama yake kuwa ameibiwa kwa kubebwa kwenye pikipiki na mtu asiyejulikana
katika eneo la Kona ya Bwiru, Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza
amepatikana baada ya kuokotwa na Wasamaria wema.
Taarifa ya leo
Aprili 21, 2026 iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza imeeleza
kuwa mnamo Aprili 18 mama mzazi wa mtoto huyo aitwaye Neema Julius
Sesela, mwenye umri wa miaka 19, mama lishe na mkazi wa mtaa wa Nyampala
“B”, Kata ya Nyamanoro, Wilaya ya Ilemela aliripoti katika Kituo cha
Polisi Kirumba kuibiwa kwa mtoto huyo ambaye jina lake linahifadhiwa kwa
sababu za kisheria.
Tukio hilo lilitokea Aprili 18, 2026 mtaa wa
Barabara ya Vumbi, Kona ya Bwiru, Wilaya ya Ilemela wakati mama huyo
akiwa katika shughuli zake, aligundua kuwa mtoto ameibiwa na mtu huyo
aliyeondoka naye kwa kutumia usafiri wa pikipiki ambayo hata hivyo namba
zake za usajili hazijafahamika.
Kwa majibu wa taarifa hiyo
uchunguzi wa tukio hilo ulianza mara moja kwa kuwahoji watu mbalimbali
wenye ufahamu kuhusu tukio hilo ambapo mkazi mmoja wa eneo hilo aliweza
kutoa ‘CCTV footage’ iliyoonesha mtu mmoja wa jinsia ya kiume akitoka
katika eneo la tukio akiwa amempakia mtoto huyo kwenye pikipiki, ingawa
namba zake za usajili hazikuweza kuonekana vizuri.
Mnamo Aprili
20, 2026 majira ya saa 3:30 usiku taarifa zilipatikana kuwa mtoto huyo
alitelekezwa kwenye makaburi ya Nyasaka yaliyopo Wilayani Ilemela kabla
ya kuokolewa na Wasamaria wema na kumpeleka kwa mwenyekiti wa mtaa wa
Nyamuge, Kata ya Nyasaka ambapo alikutwa na michubuko sehemu za usoni na
kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Sekou-Toure kwa uchunguzi zaidi.
Jeshi
la Polisi lilipata taarifa na kufika kwa ajili ya uchunguzi zaidi
ambapo Mtoto huyo Wazazi wa mtoto huyo na baba mzazi aitwaye Mwankunja
Edward (30) fundi seremala, wote wakazi wa Gana, mtaa wa Nyampala “B”,
Wilaya ya Ilemela, wamemtambua mtoto huyo kuwa ni mtoto wao huku
uchunguzi wa afya ya mtoto ukiendelea kufanywa katika Hospitali hiyo.
TANGAZA NASI BIASHARA YAKO UFIKIE MAMILIONI YA WATEJA PIGA 0654414804.

0 Comments