Kapteni
Ibrahim Traoré, ambaye aliingia Madarakani kwa njia ya Mapinduzi miaka
mitatu iliyopita, amesema kuwa Waafrika wengi hawahitaji Utawala wa
Kidemokrasia na kwamba Burkina Faso ina mfumo wake wa Serikali, bila
kutoa maelezo ya mfumo huo.
Alipoingia Madarakani, Traoré
aliahidi kurejesha Utawala wa kidemokrasia ifikapo Julai 7, 2024, lakini
miezi miwili kabla ya tarehe hiyo, utawala wake wa kijeshi uliongezwa
kwa miaka mingine mitano.
Mnamo Januari, Serikali ya Ouagadougou ilitangaza kuwa inapiga marufuku vyama vyote vya kisiasa kwa nia ya kuijenga upya nchi.
Katika mahojiano Traoré alisema: “Watu wanapaswa kusahau kuhusu Demokrasia. Demokrasia si yetu.”
Alitoa
mfano kwa nchi ya Libya ambayo ilitawaliwa kwa takribani miaka 40 na
Kanali Muammar Gaddafi, ambaye alitawala kama Dikteta lakini utawala
wake uliwapatia Walibya makazi, elimu na huduma za afya bure.
Aliuawa
katika uasi ulioungwa mkono na nchi za Magharibi. Baadae nchi
iligawanywa katika serikali mbili zinazopingana na kuibuka vikundi vingi
vyenye silaha.
0 Comments