SIMBA YAICHAPA B19,KUKUTANA NA DODOMA JIJI 16 BORA

 Na Ally Mandai

Klabu ya Simba imefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe la CRDB baada ya kuibuka na ushindi mnono wa 2-0 dhidi ya B19 FC.

Mabao ya Simba yalipatikana kupitia kwa Inno Loemba dakika ya 22 na Clatous Chama dakika ya 77.

Mchezo huo wa hatua ya 32 bora ulipigwa katika dimba la Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni jijini Dar es Salaam.

B19 FC, ambayo inashiriki ligi ya Championship, ilijaribu kuonyesha upinzani lakini ilishindwa kuhimili kishindo cha Wekundu wa Msimbazi.

Baada ya ushindi huu, Simba sasa itakutana na mshindi kati ya Dodoma Jiji FC katika hatua ya 16 bora.

Mechi zilizopigwa leo Jumamosi, Machi 7, 2026, katika hatua ya 32 Bora ya Kombe la CRDB.

Namungo FC 4 – 1 Kagera Sugar

Geita Gold FC 4 – 1 Nyika FC

Pamba Jiji 2 – 1 Transit Camp

Mashujaa FC 0 – 0 KenGold FC (Mashujaa imeshinda kwa penalti 5-3).


 

Post a Comment

0 Comments