Yanga
imepoteza mechi ya mzunguko wa tatu wa Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya
kufungwa mabao 2-0 na wenyeji wao Al Ahly katika mchezo uliopigwa nchini
Misri.
Mabao ya Al Ahly yalifungwa na Mahmoud Trezeguet,
aliyepachika bao la kwanza dakika ya 45+3 kabla ya kurejea tena dakika
ya 75, na kuihakikishia timu yake ushindi muhimu.
Kwa mujibu wa
ratiba, timu hizo zitakutana tena katika mechi ya mzunguko wa nne
itakayochezwa mwishoni mwa wiki ijayo kwenye Uwanja wa New Amaan
Complex, visiwani Zanzibar.
Matokeo hayo yanaifanya Al Ahly
kuendelea kuongoza msimamo wa Kundi B kwa kufikisha pointi 7, huku Yanga
ikishika nafasi ya pili ikiwa na pointi 4. Timu za FAR Rabat na JS
Kabylie zinabaki na pointi 1 kila moja.
Mechi ya marudiano
Zanzibar inatarajiwa kuwa ya ushindani mkubwa, huku Yanga ikihitaji
matokeo chanya ili kujiweka vizuri katika mbio za kufuzu hatua
inayofuata.
0 Comments