WAJUMBE kutoka wilaya tano za Mkoa wa Dar es Salaam, wamemchagua Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Dovya, Kata ya Bunju, ambaye pia ni Mwenyekiti wa wenyeviti wa serikali za mitaa Wilaya Kinondoni, Razalous Mwakiposa maarufu kama Zimwi, kuwa Mwenyekiti wa Wenyeviti wa mkoa huo.
Aidha wajumbe hao kutoka Wilaya za Ubungo, Kinondoni, Ilala, Kigamboni na Temeke, wamemchangua Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mwongozo , wilayani Ubungo, Pipino Pipino kuwa Katibu wa Wenyeviti wa mkoa huo.
Viongozi hao wamechaguliwa Katika uchaguzi uliofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo kwa nafasi ya mwenyekiti ilijumuisha wagombea watatu ambao niJuma Abas, Consolata Rwiza na Zimwi.
Akitangaza matokeo hayo Msimamizi wa Uchaguzi Kambi Sande, amesema jumla ya wajumbe ni 37 na Zimwi amepata
kura 24, Abas kura mbili huku Rwiza akipata kura 11 ambapo jumla ya wapigakura wakuliwa 37.
"Kwa mamlaka niliyopewa ninamtangaza Razalous Mwakiposa kuwa Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Mkoa wa Dar es Salaam,"amesema Sande.
Akizungumza baada ya kuchaguliwa, Zimwi amewashukuru wajumbe kwa imani kubwa waliyompa na kwamba ajenda yake kuu katika uongozi ni kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kutetea maslahi ya wenyeviti.
Kuhusu uchaguzi wa nafasi ya katibu, Pipino ameibuka mshindi kwa kuvuna kura 20, ambapo Athuman Gereza amepata kura 17 kati ya kura 37 zilizopigwa.

0 Comments