WAKENYA WAANDAMANA KUENZI WALIOFARIKI KUPINGA MUSWADA

 Vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini Kenya wamejitokeza katika kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu maandamano mabaya ya waliofariki mwaka jana kufuatia kupinga Mswada wa Fedha wa 2024.

 

Mjini Nairobi, vijana wamejitokeza katika barabara ya Moi Avenue wakiwa wamebeba bendera za taifa huku Mjini Mombasa, hali kama hiyo imeshuhudiwa, vijana wanaonekana wamebeba bendera za taifa la Kenya, firimbi, makaratasi na mabango yenye picha za waliofariki.

Aidha wakati Maandamano hayo yakiendelea
Idadi kubwa ya polisi imeshuhudiwa jijini Nairobi na maeneo mengine ya nchi siku ya Jumatano huku Waziri wa Usalama wa Ndani Kipchumba Murkomen, pamoja na maafisa wakuu wa usalama, waliwasili Harambee House mwendo wa saa 5:30 asubuhi kufuatilia hali hiyo.

Post a Comment

0 Comments