KMC YAMFUTA KAZI KOCHA BARES

Na Ally Mandai. 

Klabu ya KMC rasmi imetangaza kumfuta kazi aliyekua kocha wa klabu hiyo Abdallah Mohamed "Bares" pamoja na benchi lake la ufundi.

Taarifa iliyotolewa na KMC imeeleza kuwa “Klabu ya KMC imekaa na kukubaliana pande zote na kufikia makubaliano ya kusitisha mkataba na kocha Abdallah Mohamed "Bares" pamoja na benchi lake la ufundi”

Aidha taaifa hiyo imeongeza kuwa Tunatambua na kuthamini jitihada walizofanya katika kuboresha utendaji wa timu, ndani na nje ya uwanja, kwa ngazi ya mchezaji
mmoja mmoja na timu kwa ujumla.

KMC leo imepoteza mchezo wake dhidi ya Mbeya City kwa mabao 3-2 na wanaburuza mkia kwenye msimamo wa ligi Kuu ya NBC wakiwa na jumla ya alama 8.


Post a Comment

0 Comments